Pages

Subscribe:

Monday 29 September 2014

JAMBAZI LAUWAWA MORO, NI BAADA YA KUKUTWA NA BUNDUKI AINA YA SMG, RISASI, IRIZI NA NGUO YA JWTZ.

 Kamanda wa polisi mkoani Morogoro  Leonald Paul akionyesha suruari  inayofanana na sare ya jeshi la JWTZ ilikouwa ikitumika katika matukio ya ujambazi na Mwantui Anton Msangai. 

Jambazi huyo alifariki dunia baada ya kupata kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali Septemba 29 mwaka huu majira ya saa 12.45 huko katika  eneo la njia panda ya Kilosa.
  Kwa mujibu wa kamanda huyo jambazi huyo alikuwa anaelekea wilayani kilosa kwaajili ya kufanya matukio  ya uharifu.
inadaiwa Septemba 26 jambazi huyo na wenzake walivamia duka moja wilayani Mvomero na kupora 700,00  na vocha za simu na kupiga risasi juu baada ya wananchi kutaka kuwakimbiza,
Kamanda huyo alisema jambazi huyo ni miongoni mwa majambazi watano waliokamatwa na polisi baada ya kufanya matukio ya uharifu mkoani Dodoma na Morogoro.
Kamanda huyo alisema jambazi huyo alikuwa na tabia ya kutumia makundi tofauti ya watu kufanya nao uharifu katika maeneo mbalimbali kisha kutoweka na kuelekea sehemu nyingine.


Kamanda huyo akionyesha bunduki aina ya SMG aliokamatwa nayo Jambazi huyo ikiwa na magazine 2 pamoja na risasi za SMG 47.

 Pia jambazi huyo alikutwa  na irizi ambayo inasadikiwa alikuwa akitumia katika matukio ya ujambazi kwa imani za kishirikina.
  WAKATI HUO HUO 





MTU  mmoja  Joseph Ngasa anashikiliwa na polisi mkoani hapa ,kwa tuhuma za kumbaka  na kumlawiti mtoto wa miaka 7 na kumsababishia kifo chake.

Kamanda wa polisi mkoani hapa Leonald Paul alisema tukio hilo limetokea Septemba 27 mwaka huu huko eneo la Bilo, tarafa ya Ngohelanga wilayani Ulanga.

Alisema  mtuhumiwa huyo alikwenda katika nyumba hiyo kutembea  na kwamba siku ya tukio alikuwa nje, ambapo mtoto huyo alimuaga mama yake anakwenda chooni kujisaidia.

Alisema kijana huyo aliposikia hivyo alimfuata mtoto huyo chooni na kumfanyia kitendo hicho ambapo mtoto huyo alifariki dunia muda mfupi badae.

Alisema mtuhumiwa huyo anadaiwa alifanya kitendo hicho kwa imani za kishirikina, na kwamba  anashikiliwa na polisi atafikishwa mahakamani mara baara ya uchunguzi kukamilika.
 


Sunday 28 September 2014

MAZISHI YA MEHTOD MENGI KUFANYIKA ALHAMISI SEPTEMBA 2 MWAKA HUU MJINI MOROGORO


Marehemu Method Mengi
Mke wa Marehemu katikati akiwa na majonzi






Vitu vilivyotolewa na Watanzania kwa ajili ya mnada



MC James Shemdoe



















































 
 
 
 
 
Mwili  wa marehemu  Method Mengi mkazi wa Kilakala manispaa ya Morogoro ambaye alikuwa akiishi na kufanya kazi nchini Marekani unatarajiwa kuwasili hapa nchini Jumatano Septemba  mosi mwaka huu ukitokea nchini Marekani.
 
Mdogo wa marehemu ambaye pia ni Diwani wa kata ya Kilakala Ribon Mkali ,alisema baada ya mwili huo kuwasili ndugu na jamaa wanaoishi Jijini Dar es Salaam watapata fulsa ya kuaga  mwili huo katika uwanja wa ndege wa Dar kisha kuanza safari kuelekea mjini Morogoro.
Aidha alisema  ratiba ya mazishi itaanza saa 5 asubuhi nyumbani kwao Kilakala kwa  chakula, saa 7 kuaga mwili huo  saa 8itafanyika ibada ya kuombea mwili huo katika  kuu la mtakatifu Patric mjini hapa na badae kuelekea katika makaburi ya Kola hili kwaajili ya kukamilisha mwili taratibu za kuhifadhi mwili huo.
 
Hata hivyo Riboni alipoulizwa juu ya uvumi uliotawala juu ya Marehemu huyo kuuwawa alisema kwa sasa hawezi kuzungumza chochote hadi ripoti ya uchunguzi juu ya kifo cha marehemu huyo itakapokabidhiwa kwa familia.
Marehemu Method  alizaliwa Julai 4,19 72 mkoani Morogoro
 alifariki Septemba 17 mwaka huu nchini Marekani,
Marehemu ameacha mke na watoto watatu,
Mungu ametoa na Mungu ametwaa kazi yake haina makosa, roho ya marehemu ipate rehemu kwa mungu , apumzike kwa amani, Ameen.