Pages

Subscribe:

Friday 31 January 2014

MANISPAA MORO YAANZA ZOEZI LA KUNG'OA MABANGO YANAYODAIWA

 Halmashauri ya manispaa ya Morogoro imeanza zoezi la kuondoa mabango yote ambayo hayajalipiwa na kampuni zao, zoezi hilo limekuja baada ya manispaa hiyo kudai zaidi ya milinini 400 katika makampuni mbalimbali yakiwemo ya Cocacola, Tigo, PPF na TBL
 Moja ya bango lilolokuwa katika eneo  ya kona ya Kilakala likiwa limefutwa kwa rangi nyeusi
 Dawa ya deni ni kulipa na si vinginevyo, tunafuta hata maandishi yalioandiskwa ukutani
 Moja ya bango lililokuwa nje ya hotela ya Hilax , bango la matangazo ya bia ya kampuni ya TBL likichanwa na mfanyakazi wa manispaa wakati wa zoezi hilo.
 Meneja tumekuja nyie pia mnadaiwa hela ya bango, '' Hilo dogo kwa benk kama hii, tupeni madai yetu tunawandikia  hundi sasa hivi, meneja wa CRDB Mapunda akimwambia mkuu wa kitengo cha mabango katika manispaa ya Morogoro Lina
 Hili ni bango la PPF likiondolewa na wafanyakazi wa Manispaa ya Morogoro kutokana na kudaiwa kodi ya bango hilo.
bango la PPF likipakiwa katika gari la manispaa kwajili ya kupelekwa yadi hadi hapo watakapolikomboa.

CHADEMA NA CCM WATANGWANA KATIKA MKUTANO WA KAMPENI ZA UDIWANI TUNGI

 Jamani nawaomba mnipatie kiungo huyu ili niweze kushirikiana naye katika kuleta maendeleo, kazi zangu mnazijua za kuwatumikia wananchi kila siku, posho yangu yote naitumia katika kuleta maendeleo ya jimbo langu, ni maneno ya Aziz Abood mbunge wa jimbo la Morogoro mjini wakti akimndai mgombe wa udiwani kata ya Tungi Deogratias Mzeru.

 Chadema mmetuchokoza, kama polisi hawatachukua hatua kwa vurugu mlizoleta leo hadi mmepiga watu basi askari wetu wa UVCCM watafanya kazi hiyo, Ali isa katibu wa CCM wilaya ya Morogoro akisema wakati wa kampeni hizo.

 Nichagueni niwatumikie nikisaidia na hili jembe la kweli Abood.
 Kwenye baraza la madiwani hakuna nafasi ya kukaa na tembo mnyama, wanakaa  binadamu, Malupu wa malupu akiwatupia madogo Chadema juu ya mgombea wao mwenye jina la Tembo
Wakati  tunagombea kura za maoni, wawili tulikuwa wawili, mimi mwalimu wa sanaa ,a Mzeru mwalimu wa Sayans sasa ameteuliwa yeye namuunga mkono mwalimu mwenzangu,nani kama  mwalimu jamani, kuna daktari  asiyepita kwa mwalimu, mwalimu ni kila kitu, tumpe kura mwalimu Mzeru jamani, maneno ya Mwaipopo wakati wa kampeni.


 Sikilizeni,  kila kitu kinaanza kwa hatua, nyie wajasilimali anzeni shughuli zenu kwa hatu ili tuweze kusaidiana, Abood akiwaambia wajasilimali wa Tungi.
 Mheshimiwa kesho tunataka kutembelea TV na Radio yako,ni mbunge wa Lindi Said akimwambia Azizi Abood.
Kikao nimefunga tuonane kesho Tungi kambini, mwenyekiti wa CCM kata ya Tungi Bingileki baada ya kumalizika kwa mkutano wa kampeni eneo la Nane Nane.

MTANGAZAJI MAARUFU KENNETH KIDAGO LYANGA, AFARIKI DUNAI

Mwandishi Kenneth Kidago Lyanga afariki dunia

Mtangazaji wa Habari za Michezo wa East Africa Radio Kenneth Kidago Lyanga amefariki dunia nyumbani kwake Mwenge Mlalakua, Jijini Dar es Salaam.

Mipango ya mazishi ya Kenneth Lyanga inafanywa na familia yake.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Kenneth Kidago Lyanga Mahala Pema Peponi.home
 
 
Kwa wakazi  mkoa wa Morogoro Kenneth Lyanga si megeni machoni mwenu na hata masikioni kutokana marehemu alishawahi kutangaza kituo cha radio cha kanisa Kataoriki mkoani Morogoro kijulikanacho kama Radio Ukweli RU.
 
uongozi wa Blog ya Morondiyohome tumepokea taarifa ya kifo chake kwa masikitiko makubwa kutokana na kwamba ni mtu tuliyefanya naye kazi.
Kazi ya Mungu haina makosa, mbela yake nyuma yetu Amina, mwanga wa milele umwangazie ee Bwana apumzike kwa amani, Amen.

UVCCM MORO WAMCHACHARUKIA MALECELA



                                  UVCCM MORO YAMTOLEA UVIVU MALECELA

 
Kutokana na malumbano yanayoendelea kati ya Wanachama wa Chama cha Mapinduzi hususani Jumuiya ya Umoja wa vijana (UVCCM) kutokana na matamko yanayoendelea kutolewa.
Ni jambo la kushangaza sana kumuona Mzee Mashuhuri na nguli wa Chama cha Mapinduzi Waziri Mkuu Mstaafu na Makamu Mwenyekiti wa CCM Mstaafu kumuunga mkono kijana aliyekiuka katiba ya Chama cha Mapinduzi na kanuni za Umoja wa Vijana Paul Makonda kutokana na kauli yake ya kuudanganya Umma kuwa tamko alilolitoa la kumkashifu Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa NEC ndugu Edward Lowassa kuwa ni la Umoja wa Vijana. Vifungu vilivyo kiukwa kikanuni na kikatiba ni vifuatavyo:-
Makonda amekiuka katiba ya CCM Ibara ya 14(4) Mwanachama yeyote atakuwa na haki zifuatazo “Haki ya kujitetea au kutoa maelezo mbele ya kikao cha CCM kinachohusika katika mashtaka yoyote yaliyotolewa juu yake. Pamoja na haki ya kukata ya kwenda katika kikao cha juu zaidi cha CCM kama kipo endapo hakuridhika na hukumu iliyotolewa”
Kwa kuwa kifungu hiki kinatoa fulsa kwa Mwanachama kujitetea juu ya tuhuma zinazomkabili.
Je Chama cha Mapinduzi kiliwahi kumuita Mh. Edward Lowassa na wengineo wote wenye kashfa za rushwa na kutangaza nia ya Urais kumhoji na kumsikiliza na Chama kufanya maamuzi? Lakini kutoa matamko kupitia kofia ya Chama ni makosa makubwa yaliyofanywa na Makonda na anapaswa awajibishwe. Tunamshangaa pia Mzee Malecela kuunga mkono mtu aliyekiuka haki za mwanachama na utaratibu wa Chama. Huu ni ukweli kuwa tegemeo la Wazee wa CCM kusimamia haki na wajibu wa Chama umetoweka.
Lakini pia Mzee Malecela anamtuhumu Edward Lowassa kuchangia harambee, kugawa tisheti na kutoa misaada katika nyumba za Ibada Kanisani na Misikitini. Mbona wapo wanachama wengi wanaofanya harambee kama hizo mfano ni Benard Membe, Sumaye, Samwel Sitta na January Makamba wao pia wanatenda matendo ayatendayo Lowassa mbona hawajatolewa matamko. Wametengeneza hadi na kalenda kama sehemu ya kujinadi mwaka 2015. Kwa nini hawakukemewa wote kwa pamoja?.Lakini pia Paul Makonda amewakashifu viongozi wetu wa dini kwa kuwafanisha na wasaka pesa kwahili tunamtaka awaombe viongozi hawa wote msamaha haraka,Vilevile ieleweka viongozi wa dini ni nguzo ya vijana wa taifa hili na uvccm inawathamini na pia tunatoa rai kwa mtanzania yoyote mwenye imani na roho ya upendo na wa dii yoyote  kufanya kazi na viongozi wa dini na kujenga nchi pamoja nao,Je Mzee Malecela anaunga mkono Paulo Makonda kuwakashifu viongozi hawa wa dini?.Tulitegemea sana Mzee kama Malecela angekemea matendo haya kwa wanachama wote lakini ameonesha chuki binafsi kwa ndugu Edward Lowassa. Lakini hatupaswi kumshangaa maana hata Hayati Mwl Nyerere aliposema kama Mzee Malecela atagombea Urais narudisha kadi ya CCM, Hatukumuelewa Mwl Nyerere alimaanisha nini lakini kwa sasa tumepata picha kamili ni jinsi mzee huyu asivyo na busara na anaweza kukizamisha chama kwa chuki zake binafsi na maneno yake ya kupotosha watanzania.
Mzee Malecela anapaswa kuomba radhi kwa Umoja wa Vijana wa CCM kwa kumuunga mkono Paul Makonda ambaye si msemaji wa UVCCM kwa mujibu wa Kanuni za Umoja wa Vijana. Wasemaji wakuu wa Jumuiya ni Mwenyekiti na Katibu kwa ridhaa ya vikao na maadhimio yaliyofanywa katika vikao wao ndo wenye mamlaka hayo. Lakini pia Makamu mwenyekiti Mboni Mwita amekana kutolitambua tamko la Umoja wa Vijana bali ni la kwake binafsi tunashangaa Mzee Malecela kwa nini anamuunga mkono Paul Makonda.
Tunatoa wito kwa Chama cha Mapinduzi kupiga marufuku matamko yote yanayoendelea nchini na kuwachukulia hatua wale wote wanaotangaza nia ya kugombea Urais kabla ya wakati na tunamuomba Mh. Mwenyekiti wa Chama ndugu Jakaya Mrisho Kikwete kukemea hali hii kwa nguvu zake zote ili kukisalimisha Chama na kuwepo kwa utii wa Kikatiba. Kuachwa kwa hali kama hii itakuza migogoro na makundi ndani ya Chama.
Imetolewa na Komredi Heri Hoza ni Kada wa muda mrefu wa UVCCM na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya baraza la Umoja wa Vijana wa ccm Mkoa wa Morogoro. Pia ni Mwenyekiti wa CCM wa tawi jipya la Chuo Kikuu huria (Morogoro branch).

Wednesday 29 January 2014

MAKONDA ANAMAWENGE, ANATAKA KUTUVURUGA UVCCM

 Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi CCM kupitia kundi la vijana Jonas Nkya akisisitiza jambo wakati akiongea na waandishi wa habari mjini Morogoro juu ya kauli za katibu wa chipukizi na hamasa Taifa Paul Makonda za kusema waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa  hafai kuwa kiongozi, wala mwenyekiti wa CCM taifa na hata pia kuwa amirijeshi mkuu  akimtuhumu kuwa fisadi ambapo  MNEC huyo amejia juu kusema kuwa amekurupuka na kauli  na kwamba sio msemaji wa UVCCM wanamshangaa.
Kama maisha ya Mjini yamemshinda aje vijijini tumpe shamba alime sio kuuza maneno ili apete fedha za kuishi, Lowasa alikuwa kiongozi kabla ya Makonda kuzaliwa, amekurupuka kuaongea kitu asichokijua na wala hana ridhaa ya kusema hayo,atolewe UVCCM atatuvuruga, Ni MNEC mwingine wa UVCCM Ramadhani Kimwaga akiongea na waandishi wa habari mjini Morogoro.

JUMUIYA ya umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi UVCCM mkoa wa Morogoro  Imemtaka katibu wa chipukizi na hamasa Taifa Paul Makonda kuaomba radhi waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa , wazee, vijana na viongozi wa dini  kwa kauli aliotoa  za uchochezi na  za kukigawa chama.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM NEC  kupitia kundi la vijana    Jonas Nkya na Ramadhani Kimwaga walisema kuwa kauli hizo si za  UVCCM ni za Makonda binafsi.
 
Nkya alisema kuwa vijana wa mkoa wa Morogoro wamehuzunishwa na matamshi ya Makonda aliotoa juzi wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kumshutumu Lowasa kuwa hafai kuwa kiongozi wan chi hii, wala kuwa amrijeshi mkuu sambamba na mwenyekiti wa CCM  Taifa.
 
‘’ UVCCM hatupo kwaajili ya kutengeneza Marais, na si jukumu letu, na wakati wake haujafika hivyo tunamshangaa Makonda kuanza kuzungumzia masuala ya Urasi  na kuwachanganua nani anafaa  na nani hafai wakati sio kazi yake na aingii katika kikao chochote cha maamuzi ya kumteua mgombea Urais’’ Alisema.
 
Alisema kuwa hakuna kikao chochote cha baraza kilichokaa na kutoa tamko kama hilo na kwamba utaratibu wa UVCCM na CCM kwa ujumla maamuzi yote hutoka katika vikao halali.
 
‘’Sisi UVCCM hatutaki kuingiza masuala binafsi na  jumuiya yetu ambayo yatapelekea kukigawa chama na jumuiya zake, hivyo vijana lazima tubadirike’’ Alisema
 
Aliwataka viongozi wa dini, vijana mbalimbali aliowatamka  pamoja na Lowasa kupuuzia kauli hiyo na kwamba UVCCM wako pamoja  viongozi wa dini, vijana mbambali na hata waziri mkuu mstaafu.
 
Kwa upande wake Kimwaga alisema kuwa kauli ya makonda ya kusema kuwa lowasa hafai kuwa kiongozi ni kukitukana chama kwa kumteua kugombea ubunge jimbo la Monduli na pia kumteua kugombea ujumbe wa NEC nafasi ambazo ni nyeti  katika chama.
 
‘’ Lowasa amekuwa kiongozi wa muda mrefu katika CCM hata kabla makonda hajazaliwa na hadi sasa, hivyo kauli za Makonda zinaonyesha ni mtu mwenye  kuweweseka na hastaili kuwa kiongozi, hivyo hakuna budi kuenguliwa katika nafasi hiyo kutokana na kushindwa kuitumikia’’ Alisema
 
Alisema kuwa kuendelea kuwepo katika nafasi hiyo makonda kutasababisha kugawa UVCCM pamoja na kukivuruga chama .
 
‘’ Mtu ukimtuhumu kuwa fisadi mla rushwa ni lazima uwe na ushahidi na kama anao basi aende kushitaki mahakamani sambamba na katika vyombo husika kama takukuru, na kama hajui aje tumwelekeze ofisi zao zilipo’’ Alisema
 
Alimshauri makonda kuja vijijini  ili wamtafutie shamba  la kulima kuliko kukaa mjini kwaajili ya kuuza maneno ili apate fedha za kumwezesha kuishi.


Tuesday 28 January 2014

MTIBWA KUANZA KULIPA WAFANYAKAZI JANUARI 30 MWAKA HUU

 Yaani siwezi kuwa mpumbavu kuwaruhusu eti mkatandike mikeka katika kiwanda cha Mtibwa mkidai fedha zenu, Ni mkuu wa wilaya ya Mvomero Antoni Mtaka wakati akiongea na wafanyakazi, wastaafu,  na wakulima wa kiwanda cha sukari cha Mtibwa wilayani humo ambao walitaka kujua muafaka wa madai yao.

 Ni lazima tujadiliane kwa makini tupate ufumbuzi, anayesema maneno yangu ni siasa, siasa haziko hapa ziko huko. Ni Dc Mtaka akiwajibu wakulima hao waliomwambia kuwa anayoongea ni siasa na kwamba hakuna utekelezaji.


 Tunachotaka hapa leo ni kulipwa fedha zetu na sio vinginavyo, ni mmoja wa wakulima wa miwa  Mtibwa Turiani akiongea katika mkutano huo wa maelfu ya watu.

Tufanye hivi leo ni Jumanne, hawa watu tuanze kuwalipa ifikapo Alhamisi au unasemaje? meneja msaidizi Kiula akinong'ona na meneja mkuu wa kiwanda hicho Hamad Yahaya.

Monday 27 January 2014

MKE WA MASHISHANGA AFARIKI DUNIA,

 Familia ya Mzee Steven Mashishanga wakiwa katika maombolezo ya msiba wa mke wa Mashishanga Suzana aliyefariki jana. Rais  Kikwete naye alipata fulsa ya kumtembela Mgane ashishanga na kutoa rambirambi zake.
 Pole sana Mzee, Mungu akupe nguvu, sio jambo jepesi, ni kazi ya Mungu jipe Moyo Utashinda, Bwana ametoa na leo ametwaa jin lake lihimidiwe, amina, Ni katibu wa CCM mkoa wa Morogoro akimwambia Mzee Mashishanga huku akiwa amemkumbatia.
Mzee Mashishanga akiwa amejiinamia katika msiba huo, Mbele yake nyuma yetu, amina.

KIKWETE ATAKA KUPATIWA TAARIFA SAHIHI YA WAHANGA WA MAFURIKO KWA MAJINA IFIKAPO KESHO, ATILIA MASHAKA TAARIFA ALIOSOMEWA LEO NA RC MOROGORO

 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete alipowasili katika eneo la Dumila wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro kwaajili ya kuwatembelea wahanga wa mafuriko na kujionea hali halisi.
 Rais Kikwete akitembela maeneo mbalimbali yaliokubwa na mafuriko hayo.
 Rais  Kikwete akiwa katika daraja la Mto mkundi lilopo Dumila Kilosa ambalo lilikatika kutokana na mafuriko.
 Nilazima tuangalie jinsi gani ya kufanya ili kuzuia mafuriko haya yasiwe na athari kubwa kama hizi. Kikwete akitoa malekezo kwa viongozi wa mkoa na wilaya za Gairo, Kilosa na Mvomero ambazo zimekubwa na mafuriko hayo.

 Mheshimiwa mimi ni muhaisis wa chama miaka dahali sasa, nimekubwa na mafuriko kila kitu changu kimesombwa hadi kadi yangu ya chama, Salma Matewele akimwambia Kikwete.
 jamani poleni sana na mafuriko yaliowakubwa, kikwete akiwaambia wahanga wa mafuriko hayo katika eneo la Magole ambako ndiko walipoweka katika kambi.
 Mheshimiwa hapa tuna kontena tatu za dawa, hakunatatizo kabisa, mganga mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Mtei akimwambia kikwete.

 Wananchi waliofurika katika eneo la Mateteni kwaajili ya kumsikiliza kikwete kufutia mafuriko hayo.
katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Rojas Romuli akiwa na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilosa nasoro Udelele 

RAIS Jakaya Kikwete amewabana  wakurugenzi wa halmahsuri na wakuu wa wilaya za Kilosa, Mvomero na Gairo kuandaa taarifa sahihi ya wananchi walioathirika na mafuriko kwa idadi sahihi sambamba na majina ya wananchi hao  na kutaka apatiwe taarifa hiyo kesho mapema.

Rais Kikwete alisema hayo Janauri 27 mwaka huu wakati alipotembela katika eneo la Magole wilayani  Kilosa kuwapa pole wahanga hao na kujionea hali halisi ya mafuriko hayo.

Kikwete alisema kuwa kutokuwa na takwimu sahihi  na majina ya watu hao kutasababisha misaada hiyo kuwafikia  watu ambao hawajaathirika na hivyo kushindwa kuwafikia wahanga halisi.

‘’  Ni lazima mjiridhishe  kwa kuwatambua watu kwa majina na jinsia zao, hivi nikisema sasa hivi mkanionyeshe hao watu wapo’’ Alihoji Rais.

Alisema amelazimika kusema hayo baada ya mkuu wa mkoa wa Morogoro  Joel Bendara kusoma taarifa ya maafa hayo kuwa hadi sasa wananchi wapatao 12472 hawana makazi ya kuishi kutokana na mafuriko  huku akidai kuwa , idadi ya kaya zilizoathirika 2759,nyumba zilizozungukwa na maji 2922 na nyumba zilizobomoka ni  1141.

Alisema kuwa kutokuwa  na majina hayo kunamtia mashaka yeye kuwa takwimu hizo huenda sio sahihi jambo lililomfanya kuwataka kuhakiki upya na kutoa taarifa hiyo ifikapo Kesho.

‘’Uongozi unapimwa wakati wa matatizo, kutokuwa na majina na idadi sahihi kunaonyesha jinsi  gani msivyowajibika katika kutekeleza majukumu yenu’’ alisema.

Alisema kuwa  wakati wa mafuriko kama hayo yaliotokea mwaka 2009 wilayani Kilosa Mkuu wa wilaya wa wakati huo Halima Dendegu aliweza kufanya vizuri  kwa kuwa na idadi sahihi na kamili.

‘’ Halima alifanya vizuri wakati ule  japo alikuwa mwanamke, nyie hapa wanaume mnashindwa , wakati ule Halima alisimamia vizuri mkaanza maneno yenu ya hovyo, mlimsema kwakuwa alikuwa mkali,, Alisema

Hata hivyo Kikwete aliwataka wenye viwanda vya magodoro hapa nchini wanawapatia magodoro hayo ili yaweze kutumika kwa wahanga hao na kwamba hata kama hakuna fedha watalipwa badae.

Alisema kuwa chakula kipo cha kutosha na kwamba hakuna mwananchi ambaye atakufa kwa njaa na lengo la serikali ni kuhakikisha kila mwananchi anapata hudmua muhimu kama chakula, malazi na dawa pamoja na maji safi.

Alisema kuwa serikali itahakikisha huduma hizo zote zinapatikana kwa kipindi chote hiki  ili kuokoa maisha ya wananchi hao.

Alisema kuwa alipokea taarifa kutoka kwa mganga mku wa mkoa wa Morogoro kuwa hadi sasa wametibiwa wananchi 300 na kwamba magonjwa yanayosumbua ni kichomi na nimonia ambayo yanasabishwa na kulala chini jambo ambalo tayari ameagiza kila mwananchi kupatiwa gororo ili kuepuka magonjwa hayo.

Pia aliagiza uongozi wa wakala wa barabara mkoa wa Morogoro kuhakikisha wanatoa magogo na miti ilioziba katika mito na mifereji ili kuepuka maafa kama hayo katika kipindi hiki ambacho mvua zinaendela kunyesha.

Alisema kuwa mafuriko kama hayo sio mara ya kwanza kutokea kwa wilaya ya kilosa hivyo ni lazima wananchi na serikali kwa ujumla ikachukua tahadhari  ili kuepuka maafa kama hayo kutokea.
Kwa upande mwingine Rais huyo alisema kuwa atayatumia majeshi ya hapa nchini katika ujenzi wa nyumba za muda badala ya kuzitumia halmashauri ambazo zimekuwa na milolongo mingi  ambayo itatoa mianya ya wizi wa vifaa hivyo vya waathirika.

‘’ Ukizitumia halmashauri  waanze kutangaza zabuni, hapo bado watu hawajafikiria  kila mtu atapata nini, hakuna kitakachofanyika, wanajeshi hao tuliwatumia  hata katika mafuriko ya 2009 yaliotokea Kilosa na walifanya vizuri na sasa tutawatumia tena alisema.

Awali mkuu wa mkoa wa Morogoro alisema kuwa tayari walishanza kupokea misaada mbalimbali ikiwamo ya  milioni 50,000 kutoka ofisi ya waziri mkuu, milioni 10,000 kutoka Islamic Foundationi sambamba na dawa  za milioni 80,000 kwaajili ya magonjwa mbalimbali.



Friday 24 January 2014

Mawasiliano Dodoma na Morogoro yarejea baada ya daraja la Dumila kukamilika




 Waziri wa ujenzi John Magufuli akiruhusu  Lori la kwanza kupita katika daraja la Dumila wilayani Kilosa  baada ya mainjinia wa wizara hiyo kukesha  usiku kucha kutengeneza daraja hilo.

 Waziri Magufuli bakitoa maagizo katika daraja hilo.
 Magufuli akihimiza kukamilika kwa kazi ya daraja hilo ili magari yaweze kupita.

Thursday 23 January 2014

WAZIRI MKUU ANENA KWA WAHANGA WA MAFURIKO DUMILA

WAZIRI mkuu Mizengo amesema kuwa serikali imechukua hatua za dharuala kwa kuhakikisha waathirika wa mafuriko wilayani Kilosa na Mvomero wanapatiwa chakula na dawa huku serikali ikiangalia taratibu zingine za kuwahifadhi waathirika hao katika mahema.
Pinda alisema hayo januari 23 mwaka huu alipotembelea katika eneo la Dumila  na eneo la Magole kuongea na waathirika hao na kujionea hali halisi.
Alisema kuwa tayari serikali kupitia kitengo cha maafa kimeshanza kuchukua hatua za kupeleka chakula  na dawa katika maeneo hayo na kwamba amewahakikishia wananchi walioathirika kuwa watapata chakuala katika kipindi chote ili kuokoa maisha yao.
Hata hivyo waziri huyo alisema kuwa serikali itatumia majeshi yake katika kuhakikisha wananchi hao wanapata makazi ya muda .
‘’ Tunaongea na majeshi ili kuja kutusaidia katika suala la kujenga mahema kwaajili ya maafa haya, wao ndio wataalamu  tunaamini watatusaidia sana.
Alisema kuwa mafuriko hayo ni makubwa sana ambayo yaliwahi kutokea miaka zaidi ya 15 iliopita wilayani Kilosa  mkoani hapa.
Alisema kuwa mafuriko hayo yamekuwa makubwa kutokana na  barabara hiyo ya Morogoro  na Dodoma kuinuliwa  na kuwa kama tuta hali inayosababisha maji kubakia upande mmoja na hivyo kuathiri zaidi.
‘’ Barabara hii ingekuwa kama ilivyokuwa awali maafa yasingekuwa makubwa kama hivi, hivyo kuna kila sababu ya kuangalia jinsi gani watahakikisha wanaondokana na tatizo hilo ‘’ Alisema
Alisema  kuwa serikali imeshaanza kuchukua hatua kupitia kampuni ya ujenzi ya wachina ya wilayani  Kilosa kuweza kujenga daraja hilo ili maroli na magari mengine ambayo yamekwama kuweza kupita na kuendela na safari yake.
‘’ Tumeongea nao wametuahidi watatumia siku nne kujaza mawe ili barabara hiyo iweze kupitika lakini tumewaomba wajitahidi kutumia siku tatu ili kupunguza adha ya wasafirishaji hao’’alisema.
Alisema kuwa kampuni hiyo ya wachina ilishaanza kazi hiyo na kwamba hadi sasa wameshamwaga roli 150 za mawe kwa upande wa Morogoro na wanaendela upande wa Dododma ili kukamilisha kazi hiyo.
Kwa upande wao madereva wa maroli na utigo wao walidai kuwa wanakabiliwa na tatizo la kushindwa kulala kwa kuhofia kuibiwa hivyo kulazimika kukesha wakilinda maroli yao.
‘’ Yaani hapa usiku mzima hatulali tunalala mchana kwani eneo lenyewe sio salama na magari  hayo unayoona zaidi ya 300 tunaogopa kuibiwa ‘’ Alisema Isa Ramadhani mmoja wa utingo wa roli.
Juma Musa mfanyabishara wa mahindi katika eneo hilo la Dumila alisema kuwa kwa sasa biashara imekuwa nzuri kutokana na bidhaa kuuza kwa bei mara mbili ya awali.
Alisema kuwa mahindi ya kuchoma yaliotakiwa kuuzwa shilingi 300 hadi 500 huuzwa kwa shilingi 1000 na ndizi za kuiva zinazouzwa shilingi 100 huuzwa 200 hadi 300.
Nao wananchi wa eneo la Magole walioathirika na mafuriko hayo walidai kuwa vitu vyote vimesomba na maji hivyo hawana mahali pa kulala wala chakula na kwamba tangu jana hawajala kitu.
‘’ Tangu jana tunatabika hatujala kitu, vyakula, mifugo, vyombo vimesmombwa na maji’’ Alisema Mwajuma Omari.
Chama cha Mapinduzi CCm Mkoa wa Morogoro kimesema kuwa  kimepokea taarifa hiyo  ya maafa kwa masikitiko makubwa na kwenda kujionea hali halisi .
Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro alisema kuwa wameipongeza serikali kwa hatua za haraka wanazochukua kuwasaidia wananchi hao na kuiomba iendelee kuwasaidia ili kunusuru maisha yao.
Wakati huo huo Waziri mkuu huyo alisema kuwa  Rais  Jakaya Kikwete alituma salama za pole kwa wahanga wa mafuriko hayo na kuahidi kuwa serikali itakuwa bega kwa bega nao katika kipindi hiki ili kuhakikisha wanaokoa maisha ya watu hao na kuona uwezekano wa kuwapatia mahitaji muhimu.
Mwisho