Pages

Subscribe:

Wednesday 15 January 2014

CCM MORO MJINI YAWATAKA WALIOGOMBEA UDIWANI TUNGI KUUNGA MKONO ALIYETEULIWA .


 Mgombea udiwani kata ya Tungi manispaa ya Morogoro kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Deogratias Mzeru akikabidhi fomu ya kuwania udiwani kwa mtendaji wa kata hiyo Abuu Liwangira Januari 15 mwaka huu.
 Mgombea Udiwani Mzeru akikabidhi fomu zake kwa mtendaji wa kata ya Tungi mbela ya katibu wa CCm wilaya ya morogoro mjini Ali Isa.
 Hongera Mzeru, tumekuja kukuunga mkono wenzako, ni wagombea udiwani wa kata ya Tungi Lusajo Manase na Godfrey Taiko .
 Tuko pamoja na ushindi ni lazima, mimi niko CCM muda mrefu sana hivyo lazima tuhakikishe CCM inashinda Tungi. Godfrey Taiko akimwambia mgombe mwenzake Mzeru waliomsindikiza kuchukua fomu ya kuingia katika kinyang'anyiro hicho.
 Pamoja sana Mzeru, tumekuja kukusindikiza , CCM ushindi ni lazima.
 katibu kata  wa CCM kata ya Tungi Zulfa akiwa katika picha ya pamoja na wagombea udiwani wa kata hiyo.
 Nani kasema imekaa vibaya, CCM imekaa vizuri, . Mzeru amekaa vizuri. jeshi la CCM ndani ya Tungi.
 Mnajua sisi wanawake lazima tuhakikishe kinaeleweka hapa Tungi ama sivyo jamani, katibu wa UWT Dotto akiwaambia wanawake wa manispaa ya Morogoro
 Vijana wa CCM wakia nje ya ofisi ya mtendaji wa kata ya Tungi wakisubiri mgombea udiwani Mzeru kurejesha fomu.
 Hatutaki matusi, wala kejeri katika uchaguzi huu, kila chama kinadi sera zake, wananchi wanahitaji sera na maendeleo na sio matusi, Mgombea udiwani kata ya Tungi kwa tiketi ya chama cha Jahazi Asilia Ismail Ismail . alipofika katika ofisi ya kata na kuongea na wanachama wa CCM.
 Makada wa CCM wakijadiliana nje ya ofisi ya mtendaji kata ya Tungi
 Viongozi wa CCM wilaya ya Morogoro mjini wakisubiri mgombea wao Mzeru kurejesha fomu nje ya ofisi ya mtendaji kata ya Tungi.
Wananchi wa kata ya Tungi waliomsindikiza mgombea wao Mzeru kurejesha fomu wakiwa katika picha ya pamoja.



CHAMA cha mapinduzi CCM wilaya ya Morogoro kimewataka wagombea udiwani katika kata ya Tungi Manispaa ya Morogoro ambao hawakuteuliwa kushirikiana na mgombea aliyeteuliwa katika kukupatia ushindi wa kishindo.
Katibu wa CCm wilaya hiyo Ali Isa alisema hayo jana wakati akiongea na baadhi ya wagombea hao katika kata ya Tungi mara baada ya Mgombe udiwani aliyeteuliwa na CCM Deogratias Mzeru kurejesha fomu katika ofisi ya mtendaji kata wa Tungi.
Alisema kuwa CCm inautaratibu katika mchakato wa kupata viongozi na kwamba katika mchakato huo wagombea ambao hawakuteuliwa wasikate tamaa.
Alisema kuwa CCM itaanza mikutano yake ya ndani Januari 16 mwaka hu na kwamba wanatarajia kuzindia kampeni rasmi januari 26 mwaka huu ambapo mgeni Rasmi atakuwa Asha Rose Migiro ambaye ndio mlezi wa wilaya hiyo.
‘’ wagombea ambao hawakupata fulsa ya kuteuliwa nawaomba washirikiane katika kumnadi huyo aliyeteuliwa ili CCM ishinde kwa kishindo’’ Alisema.
Kwa upande wao wagombea hao Godfrey Taiko alisema kuwa yeye ni kada wa siku nyingi ndani ya CCm na kwamba kutoteuliwa katika nafasi hiyo hakuwezi kumfanya akakisaliti chama na kwamba nafasi ziko nyingi anaimani atapata nafasi zingine.
Naye Lusajo Mwambogo alisema kuwa atashirikiana vizuri katika kumnadi mgombe huyo ili kuhakikisha CCm inashinda kwa lengo la kuletea maendeleo kata hiyo ya Tungi.
Uchaguzi huo umekuja baada ya diwani wa kata hiyo Daud Mbao kufariki dunia kutokana na kuugua kwa muda mrefu Ugonjwa wa Kisukari.


0 comments:

Post a Comment