Pages

Subscribe:

Wednesday 16 July 2014

RC MORO AKEMEA WANAOTUMIA VIBAYA MITANDO YA KIJAMII.


 Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akifungua mkutano wa 98 wa watayarishaji wa vipindi shirika la utangazaji la Taifa TBC.


Baadhi ya washiriki wa mkutano huo.



MKUU wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera amewataka watumiaji wa mitandao  ya kijamii ,  kuacha tabia ya kutumia mitandao hiyo kwaajili ya kukashfiana , kutoleana lugha chafu na  kudhalilishana na badala yake itumike kwaajili ya kutoa elimu na burudani.


Alisema hayo jana wakati  wa mkutano wa 98 wa watayarishaji wa vipindi vya elimu kwa umma kupitia shirika la Utangazaji Tanzania TBC.


Alisema mitandao hiyo kwa sasa watumiji wamekuwa wakitumia kinyume na malengo, kutokana na kukosa nafasi katika vipindi mbalimbali vya Tv na radio.


‘’ Mara nyingi mashirika ya utangazaji yamekuwa yakitoa nafasi kwa wataalam na viongozi  huku waiwasahau wananchi jambo linalosababisha kutumia mitandao ya kijamii kuweka habari zao’’ alisema


Hata hivyo mkuu huyo aliwataka watoa habari kuacha tabia ya kukwepa kutoa habari kwa waandishi wa habari pale zinapohitajika kwani kufanya hivyo kunasababisha kuandikwa kwa habari zisizo sahihi.


‘’ waandishi wa habari sio watu wa kuwakimbia, wanapohitaji habari wapatie ili waweze kuchuja na kuandika kile kinachofaa’’ Alisema


Hata hivyo aliwataka waandishi wa habari kuacha tabia ya kuandika habari kwa  zenye chuki na kulenga kumdhalilisha mtu bila sababu yeyote.


Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa TBC Clement mshana aliwataka wasemaji wa wizara kujenga tabia ya kuita vyombo vyote vya habari pale wanapotaka kutoa taarifa ya uelimisha umma au zinapofanyika kampeni mbalimbali.


Alisema lengo la mafunzo hayo ni kuboresha weledi wa utayarishaji wa vipindi mbalimbali katika shirika hilo.


Kwa upande wake  mkurugenzi wa mfuko wa Pensheni wa PSPF Adam Mayingu alisema mfuko huo kwa sasa mfuko huo una wanachama tegemezi wapatao 400,000.


Alisema lengo la kudhamini mafunzo hayo ni kuwafanya watayarishaji hao kuwa na uelewa juu ya  mfuko huo wa PSPF .


0 comments:

Post a Comment