Pages

Subscribe:

Monday 17 February 2014

ALAT YATISHIA KUGOMEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KAMA KATIBA MPYA HAITAWATAMBUA KIKAMILIFU

 Mwenyekiti wa jumuiya ya serikali za Mitaa ALAT Taifa Didas Masaburi kulia, meya wa manispaa ya Morogoro ambaye pia ni mwenyekiti wa ALAT mkoa wa Morogoro Amir Juma Nondo katikati  na katibu wa ALAT Habraham Shamumoyo wakati wa kikao cha wadau wa ALAT kilichofanyika mjini Morogoro.

 Wadau wa ALAT wakiwa na viongozi wao wakuu katika picha ya pamoja
 Wajumbe wa ALAT wakifutilia mkutano huo kwa makini.
Ipo haja ya kususia uchaguzi wa serikali za mitaa kama katiba mpya haitatutamka ipasavyo, ni maneno ya Daniel Okoka makamo mwenyekiti wa ALAT Taifa.


Habari zaidi soma hapo chini.

MWENYEKITI wa jumuiya ya serikali za Mitaa Taifa ALAT Didas Masaburi  amesema kuwa wameazimia kwenda Dododma kuwaomba wabunge wakatae kukaa vikao vya kujadili rasimu ya pili ya katiba mpya  na kwamba irudishwe kwa wananchi ili iwekwe vipengele vinavyozingatia masuala ya serikali za mitaa.

Masaburi alisema hayo Februari 17 mwaka huu wakati akiongea na waandishi wa habari  baada ya kufungua mkutano wa wadau wa ALAT uliofanyika mjini Morogoro.

Alisema kuwa katika rasimu hiyo serikali  za mitaa imetamkwa kuwa itashiriki  kama nchi washiriki na kwamba haikuipa umuhimu wake.

Alisema kuwa ili wananchi wengi waweze kushiriki kikamilifu hakuna njia inayoweza kuwakutanisha isipokuwa ni serikali za mitaa.

‘’ Hakuna baraza linaloweza kuwashirikisha wananchi wakashiriki kikamilifu bali ni njia ya serikali za mitaa, lakini katika hii mpya haijaitamka ipasavyo na kwamba tunaona serikali za mitaa zimeonekana hazina umuhimu, maendeleo mengi yanafanywa kupitia serikali za mitaa sasa leo kama haijashirikishwa kikamilifu sio ndio inakosa maana’’ Alisema

Alipongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kuhakikisha miundombinu ya kitaifa imeimarika ipasavyo na kuongeza kuwa ili nchi iweze kutanuka zaidi hakuna budi kupanua miundombinu ya ndani ambayo inatokana na serikali za mitaa.

Alisema kuwa katiba hiyo ilijadiliwa kwa mfumo serikali mbili kwa maana ya Zanzibar na Tanzania na kwamba kama muundo wa Nchi tatu Watanganyika hawajashiriki hivyo katiba hiyo irejeshwe na kujadiliwa na Watanganyika.

Naye Daniel Okoka ambaye ni makamo mwenyekiti wa ALAT msingi wa serikali kuu ni serikali za mitaa hivyo kama serikali za mitaa hazitambuliki hakuna umuhimu wa kuwepo hata hao viongozi wa ngazi hizo.

‘’ Kwa kuwa kuna uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu , kama hawatatutambua katika katiba basi tutasuasia uchaguzi huo ‘’ Alisema

Naye katibu mkuu wa ALAT Habubakar  Shamumoyo alisema kuwa lazima  kuwepo na vipengele vinavyoelezea misingi, kanuni na masharti ya ung’atuaji wa madaraka kupeleka kwa wananchi.

Alisema kuwa kama alat ilitoa mapendekezo yake ili yaingie katika katiba hiyo lakini hayakuzingatiwa na badala yake kimetamkwa kipengele kidogo.

0 comments:

Post a Comment