Pages

Subscribe:

Wednesday 5 February 2014

UVCCM MORO YAPINGA TAMKO LA MWENYEKITI MKOA MOROGORO, YASEMA NI LAKE BINAFSI, HALINA BARAKA ZA VIKAO, WAENDELEA KUMSISITIZA MALECELA KUOMBA RADHI UVCCM .





 







Ndugu zangu waandishi wa habari

Habari za kazi, na hongereni sana kwa kazi nzuri ya habari mnayoifanya katika jamii yetu.



Ndugu zangu nimewaiteni hapa ili kusema machache na kuendelea kutoa maoni yangu binafsi kama mwanachama hai wa Umoja wa vijana (Uvccm) kuhusu kumsisitiza mzee John Samwel Malecela auombe radhi Umoja wa vijana waTanzania kwa kitendo chake cha kuunga mkono tamko lilitolewa na mkuu wa idara ya uhamasishaji na chipukizi wa uvccm Tanzania Ndg Paul Makonda,,


Msisitizo wangu unatokana na jinsi gani nilivyosikitishwa na kitendo alichokifanya Mzee Malekela cha kumuunga mkono ndg Makonda,, ambae tamko lake limekataliwa na Mwenyekiti wetu wa Taifa ndg  Sadifa Juma Khamis, kwamba si la umoja wa vijana na si vema kwa wanachama kusemana nje ya vikao, pia makamu mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Tanzania Ndg Mboni Muhita pia amelikataa ya kwamba halitokani na Umoja wa vijana, ikumbukwe kwamba Makamu Mwenyekiti ni mtu wa pili kiitifaki katika umoja wa vijana ukilinganisha na Ndg makonda ambae ni watano katika uvccm. Na ni kiongozi wa idara tu. Mzee malekela kuliunga tamko la Makonda ni kinyume cha utaratibu na amewakosea heshima viongoz wetu wa vijana wa taifa na uvccm yote kwa ujumla.

Mbali na hilo, pia tamko la ndg Makonda limebeba misamiati tata ambayo imesababisha mgongano wa hoja baina ya viongoz wa kiimani na waumini wao wa madhehebu yote ambayo pia ni sehemu ya taifa hili.. mgongano huo wa viongoz wa kiimani na Chama unaweza ukakiathiri Chama chetu kwa kiasi kikubwa.

Ni rahisi sana kwa viongozi wa kiimani kumsamehe ndg Makonda kutoka na rika lake, lakini ni vigumu sana kumuelewa Mzee wa chama kwa kuunga mkono na wanaweza wakahisi kwamba chama kimemtuma ndg Makonda kwenda kuwahusisha katika tamko lake, jambo ambalo sio la kweli. Lkn pia nasikitishwa sana kumuona Mzee wetu huyu kuunga mkono tamko linalomdhalilisha mkt wetu wa vijana taifa na watendaji wake kwa mtu mmoja kuivunja kanuni mbele yao, huku akiudanganya umma kwamba ni tamko la Uvccm..

Ndugu zangu waandishi, naendelea kusisitiza kwamba Mzee Malecela auombe radhi umoja wa vijana Tanzania..

Pamoja na hayo,, pia napenda kutoa maoni yangu binafsi kuhusu maelezo ya mkt wa uvccm mkoa wa Morogoro aliyoyatoa jana kwa waandishi wa habari, yale yalikuwa ni mawazo yake binafsi na sio ya umoja wa vijana kwakuwa hayajapitia katika kikao cha kamati ya utekelezaji cha mkoa,, amefanya vema kuujulisha umma kwamba maoni niliyoyatoa mimi awali yalikuwa ni maoni yangu binafsi na si ya uvccm mkoa kama nayeye pia maoni aliyoyatoa ni yake binafsi na si ya uvccm  mkoa waMorogoro. Na chama kinaruhusu mtu kutoa maoni yake binafsi, nampongeza sana

Lakini pia, si jambo jema kwa kila anayetoa maoni binafsi kuhusu mustakabali wa chama, kuyahusisha maoni yake na maswala ya makundi,, na chama chetu hakijamzuia mwanachama yeyote mmoja mmoja kutoa maoni yake binafsi,, tukianza kuwanyima fursa wanachama kutoa maoni yao kwa mihemko ya makundi, basi tutaikandamiza demokrasia ya ndani ya chama, kama viongoz ni lazima tujue kutofautisha kati ya vichwa vya habari vya habari na habari yenyewe, vinginevyo kutokana na ukubwa wa chama na maoni yanayotolewa na wanachama wa maeneo mbalimbali ya ndani na nje  ya nchi, kutakuwa na watu wa kukanusha au kurekebisha, na wale wa kutoa maoni, CCM ni chama cha wanachama wote,, pasiwepo namna yeyote ile ya kunyimana uhuru.


Naungana na Mwenyekiti wa uvccm mkoa wa Morogoro kumpongeza sana mkt wetu mpendwa na rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania mhe Jakaya Mrisho Kikwete kwa hotuba yake nzuri aliyoitoa mkoani Mbea hivi karibuni katika sherehe za kutimiza miaka 37 ya chama chetu imara cha CCM, ni wajibu wetu sote kuyatekeleza yale aliyotuagiza mhe mkt wetu wa CCM taifa. Na hasa kuheshimu maamuzi yatokanayo na vikao


Ndg zangu mkoa wa Morogoro umekumbwa na matatizo mengi sana, ikiwa pamoja na mapigano ya wakulima na wafugaji, na mafuriko yaliyotokea wilayani kilosa na mvomero,, nami napenda kutoa pole kwa wahanga wa matatizo hayo, na kuunga mkono maoni ya mkt wa uvccm mkoa kwa wadau mabalimbali kujitokeza katika kusaidia wahanga, pia nawapongeza sana viongozi wa serikali na chama wote kwa kuwajibika kutatua na kusaidia katika swala hili..

Lakini ni vema sana kwa sisi vijana kuwa wa kwanza na mstari wa mbele kufika katika maeneo ya matukio mapema ili kuona hali na kushiriki katika hatua za awali,, tusijifunze kutoa pole kwenye vyombo vya habari baada ya matukio kuwa yameshapita na hatujafika hata eneo lenyewe la tukio.. hapo tutakuwa tunaonekana tunafanya siasa badala ya kazi.. lakini kutoa maelekezo au wito katika maeneo ya majanga ambayo tayari mkt wetu wa taifa ameshafika na kufanya hivyo, ni makosa ambayo tunahitajika kujifunza…

Napenda sana kutoa pongez zangu binafsi kwa vijana wa uvccm wilaya ya mjini na wale wa kilosa kwa jinsi wanavyoshiriki kikamilifu katika shughuli za kampeni katika katika chaguz za marudio kata ya tungi na ludewa, ni maoni yangu binafsi kwamba na sisi wanachama wengine tushiriki kikamilifu, badala ya kutoa maoni huku tukiwa hatujawahi hata kufika katika eneo la tukio. Hasa katika maeneo amabayo kuna chaguzi za marudio ndani ya taifa letu

Pia ni maoni yangu kwa vyama siasa hususani chadema kuacha kampeni za vurugu na kujeruhiana ambazo zinawadhuru wananchi, kuwanyima amani na kuzorotesha shughuli zao za kiuchumi, tufanye kempeni za kiistarabu, za hoja na amani kama ilivyo desturi ya nchi yetu, pia vyombo vya ulinzi naviomba viongeze umakini zadi katika kipindi hiki hasa katika maeneo yale ambayo kampeni zinafanyika..

Asanteni kwa kunisikiliza, nawatakia kazi njema!!

IMETOLEWA NA

HERI HOZA
Mjumbe wa kamati yautekelezaji ya baraza la UVCCM
Mkoa wa Morogoro





0 comments:

Post a Comment