Pages

Subscribe:

Thursday 20 February 2014

MANISPAA MORO YATIA SAINI MKATABA WA MABILIONI YA FEDHA UKARABATI WA BARABARA KWA KIWANGO CHA RAMI

 Meya wa manispaa ya Morogoro Amiri Nondo akitia saini mkataba ukarabati wa barabara za Mlapako, Kingo, Kitope na Nguzo katika manispaa hiyo

 Meya huyo  akitia saini mikataba hiyo katika eneo la Barabara ya kitope maarufu kama Shani sinema.

 Meya Nondo akitia saini mkataba wa barabara ya Kingo kata ya Sabasaba  katika manispaa ya Morogoro
 Hapo utiliaji wa saini ukiendelea.
 
Meya huyo akikabidhi mkataba kwa mkandarasi wa kampuni ya C.G.I ya Morogoro.



 Jamani mkafanya kazi vizuri kwa uaminifu, ni maneno ya meya wakati akikabidhi mkataba wa ukuarabati wa barabara hizo kwa mkandarasi wa kampuni ya barabara ya Victoria.
 Meya huyo akikata utepe katika barabara ya Kitope kama ishara ya kuzindua ujezni huo
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Morogoro Mjini Fikiri Juma akishuhudia uzinduzi  huo katika eneo la  barabara ya Kitope





 meya huyo akiwa na viongozi wa manispaa katika eneo la Uruguru
 Hali ilivyo sasa katika barabra ya Kitope ambayo itaanza kukarabatiwa hivi karibuni
 Meya huyo akielezea jinsi mikataba hiyo inavyotakiwa kuanza na kumalizika kwa wakati


HALMASHAURI ya manispaa ya Morogoro imetia saini mkataba wa ujenzi wa barabara tano zenye urefu wa kilomita 1.48 kwa kiwango cha rami kwa gharama ya shilingi bilioni 1,148,932,800   na kampuni ya C.G.I  ya mkoani hapa.

Meya wa manispaa ya Morogoro Amiri Nondo alisaini mkataba huo jana katika eneo la barabara ya Kitope na kuukabidhi kwa kampuni hiyo kwaajili ya kuanza ujenzi huo.

Meya huyo alisema kuwa ujenzi huo unatarajiwa kuanza Februari 27 mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Julai 18 mwaka huu.

Aidha alisema kuwa barabara zitakazohusika na ujenzi huo wa kiwango cha rami ni pamoja na Barabara ya Mlapakolo, Kingo , Kitope hadi posta , Nguzo hadi barabara ya Boma , Morogoro sekondari shule ua msingi Bungo.

Pia manispaa hiyo imetiliana saini na kampuni zingine tatu kwaajili ya ujenzi wa barabara katika kata ya Boma, Tungi Mji Mkuu  kwa kiwango cha Changarawe.

Alisema kuwa kampuni hizo ni SHilo Construction Co. Ltd ya mjini hapa ambayo itajenga barabara ya Uruguru kilomita 0.733 kwa kiwango cha changarawe kwa gharama ya shilingi 71,299,500 na ujenzi wake utaanza februari 27 na kumalizika Mei 19 mwaka huu.

Alitaja kampuni nyingine kuwa ni Victoria Earth Plan ya mjini hapa ambayo itakarabati barabara ya Rwegasore kilomita 1.063 kwa kiwango cha Changarawe. Kwa gharama ya shilingi  milioni 159,321,150  ambapo ujeniz wake unatarajia kuanza Februari 27 mwaka huu na kumalizika Mei 19 mwaka huu .

Meya huyo aliwataka wananchi katika manispaa hiyo kutoa ushirikiano kwa wakandarasi hao ili kuepuka vitendo vya kuhujumu vinavyoweza kufanywa na baadhi ya wanancho wasio waaminifu.

Kwa upande wake injinia wa manispaa ya Morogoro Abdul  Digaga alisema kuwa katika ujenzi wa barabara hizo watafanya zoezi la bomoa bomoa kwa wamiliki wa nyumba waliojenga ndani ya barabara ili kupisha zoezi hilo kufanyika kwa ufanisi.

Kwa upande wake madiwani wa kata ya Mjini mkuu Hasan Maringo alisema utiliaji saini mikataba hiyo ni utekelezaji wa ahadi ambazo madiwani hao waliahidi kwa wananchi  na kwamba ni moja ya utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi.




0 comments:

Post a Comment