Pages

Subscribe:

Saturday 22 February 2014

ASKOFU MORO AOMBA SERIKALI KUWAONDOLEA KODI KATIKA VIFAA VYA HUDUMA ZA AFYA

 Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera akizungumza katika uzinduzi wa kituo cha afya cha Mtakatifu Thomas kilichopo kata ya kilakala manispaa ya Morogoro.
 Askofu wa jimbo katoriki la Morogoro Telesphori Mkude akizungumza katika hafla hiyo

 Mkuu wa wilaya ya Morogoro Said Amazni naye alipata fulsa ya kuzungumza katika hafla hiyo.

 Diwani wa kata ya Kilakala akielezea jinsi walivyofarijika kupata kituo hicho.

 Mkuu wa mkoa wa Morogoro Bendera akiwa na viongozi wenzake katika picha ya pamoja.

 Mkuu wa shirika la damu takatifu sista Claudia Maria akielezea historia ya kituo hicho.

 Hii ni moja ya wodi ya wanaume katika kituo hicho.

 Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera akizunguka kukagua mazingira ya kituo hicho

 Wauguzi na wananchi wa eneo la jirani na kituo hicho wakifurahia katika uzinduzi huo.

 Ulifika wakati wa kufungua muziki, viongozi hao waliondoka na miondoka ya mfano wa nyimbo za kabila la Kichaga wanaoshikana mikono .

Namie sikuwa mbali sanaa, hao wabibi nimekuwa nao tangu utoto wangu, tulikuwa tukisali pamoja katika kanisa la Kituo hicho, Tulikuwa wote katika Rejio Maria, nilifarijika sana nilipowaona nikaona niweke kumbukumbu.

Habari kamili soma hapa


ASKOFU wa jimbo Katoriki la Morogoro Teresphori Mkude ameomba serikali kuwasaidia kuwaondolea kodi  kwa vifaa vya huduma za afya  wanavyoingiza ili waweze kuboresha zahanati na vituo vya afya katika jimbo hilo.

Alisema hayo jana wakati wa uzinduzi wa kituo cha afya cha St Thomas kilichopo kata ya Kilakala katika manispaa ya Morogoro.

Alisema kuwa wanafikiria zaidi kuboresha huduma ya afya hususani vijijini na kwamba ili wafanikiwe  hakuna budi kwa serikali kuangalia uwezekano wa kuwaondolea kodi hiyo.

Alisema kuwa tayari wameshaomba wafadhili kutoka nje kwaajili ya kuwasaidia vitanda vitatu kwaajili ya kujifungulia wajawazito  ili waweze kupeleka katika zahanati yao iliopo Maskati Turiani wilayani Mvomero.

Pia aliomba serikali ya wilaya ya Mvomero kuwaboreshea barabara ya kwenda Maskati ili iweze kufikika kwa nyakati zote na kuweza kuwasaidia wagonjwa kufika katika zahanati hiyo kwa urahisi.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Morogoro ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo alisema kuwa  Serikali inafarijika kuona mashirika ya dini yanapotoa huduma hizo  ambapo aliwahakikishia kuwa nao bega kwa bega katika kufanikisha huduma hizo.

‘’ Tangu miaka ya zamani mashirika ya dini ndio yaliweza kutoa huduma bora zaidi za afya na elimu, na tunatambua mchango wenu ndio maana hata mnapohitaji watumishi hatusiti kuwapatia’’ Alisema

Naye mkuu wa shirika la damu takatifu linalomiliki Kituo hicho cha Afya sista Claudia Maria alisema kuwa kituo hicho kilianzishwa mwaka 1982 kama zahanati ambayo ilikuwa ikitoa huduma  kwa wagonjwa wa nje .

Alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa huduma hiyo kwa wananchi wa manispaa ya Morogoro waliamua kuboresha na kukipandisha hadi hadi kufikia kituo cha afya .

Alisema kuwa kwa sasa  wanampango wa kujenga chumba cha upasuaji ili wajawazito wanaopatwa na matatizo waweze kupata huduma hiyo hapo.

Alisema kuwa kituo hicho  kinahudumia wagonjwa 1074 kati ya hao 289 ni wa mfuko wa bima ya afya na kuongeza kuwa changamoto walionayo ni mfuko huo kuchelewesha malipo na  kusababisha upungufu wa dawa .




0 comments:

Post a Comment