Pages

Subscribe:

Friday 14 February 2014

AJIRA HIZI HAPA: WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI IDARA YA UHAMIAJI


Kamishna Mkuu wa idara ya Uhamiaji anatangaza nafasi za kazi katika Idara ya Uhamiaji kwenye
vyeo vya Koplo na Konstebo wa uhamiaji.

A: MKAGUZI MSAIDIZI WA UHAMIAJI NAFASI 70
1. SIFAZINAZOHITAJIKA
Awe na shahada ya kwanza au Stashahada ya juu kutooka vyuo vikuu vinavyotambuliwa na serikali katika fani zifuatazo; Sheria, Uchumi, Biashara, Utawala, Uandishi wa habari, Ualimu, Usafirishaji, Rasilimali watu, Sayansi ya kompyuta, Teknolojia ya mawasiliano, Takwimu, Uchapaji, Uhandisi majengo na Uhandisi Mitambo.
Awe na umri usiozidi miaka 35
2. MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA
(i) Kusimamia doria sehemu za mipakani, Bandarini, Vituo vya Mabasi, Treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini vikiwemo vya majini.
(ii) Kusimamia shughuli za upelelezi, kuandaa hati ya mashitaka na kuendesha mashitaka.
(iii) Kutoa na kupokea fomu mbali mbali za maombi ya hati za uhamiaji
(iv) kufanya ukaguzi wa mwanzo wa maombi mbalimbali
(v) kupokea na kukagua hati za safari, fomu ya kuingia na kutoka nchini.
(vi) kuidhinisha malipo mbalimbali ya huduma za uhamiaji kwa wanaostahili
(vii) kuagiza ufunguaji wa majalada ya watumiaji
(viii) kutunza kumbukumbu za ruhusa kwa wanaongia na kutoka nchini
(ix) kukusanya, kusimamia na kutunza takwimu za uhamiaji na uraia

(x) Kuandaa majibu ya maombi yote ya huduma za uhamiaji yaliyokubaliwa au kukataliwaZINAENDELEA

0 comments:

Post a Comment