Pages

Subscribe:

Friday 18 April 2014

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA MVOMERO ATISHIWA KUBAMBIKIZIWA KESI


MWENYEKITI wa Halmashauri ya wilaya ya Mvomero Jonas Zee Land amelalamikia kutishiwa  na baadhi ya wanasiasa katika wilaya hiyo kuwa watambambikizia kesi kufutia mgogoro uliokuwepo baina ya madiwani wa wilaya hiyo na mwenyekiti wa umoja wa vijana UVCCM Paskari Boga  wilaya hiyo.

Alisema hayo jana wakati akiongea na waandishi wa habari juu ya vitisho anavyopata kupitia ujumbe uonaotumwa katika mitandoa ya simu za mkononi.

‘’ Nimetumiwa ujumbe ,’’Suala la madiwani na mwenyekiti wa UVCCM unachochewa na Jonas na nimemwagiza Lule ahakikishe  Jonas na wapambe wake wote tunawavuruga na  kuwabambizia kesi mambo mengi nitawapa napita hapo jumapili tukutane’’ alisema

Alisema kuwa kwa muda sasa wilaya hiyo imegubikwa na mgogoro baina ya mwenyekiti huyo na madiwani baada ya mwenyekiti huyo kuwaita madiwani hao mizigo.

Alisema ameamua kuweka wazi vitisho hivyo ili jamii na vyombo vya usalama vijue na kongeza kuwa tayari alishatoa taarifa polisi dhidi ya vitisho hivyo.

Alisema mgogoro uliokuwepo baina ya mwenyekuti huyo wa UVCCM na balaza la madiwani ni kwamba aliwaita madiwani wa wilaya hiyo kuwa ni mizigo, viwete na kuwataka vijana kutowachagua kutokana na kushindwa kusimamia asilimia 10 ya mapato ya halmashauri  inayotakiwa kupewa mikopo kwa vijana na wanawake.

Jonas alisema baada ya matamshi hayo walikaa balaza la madiwani na kutoa maazimio  wapeleke taarifa hizo kwenye chama ili hatua za kinidhamu zichukuliwe ikiwa ni pamoja na kumtaka akanushe ndani ya siku 14 kama atashindwa kuthibitisha juu ya usemi wake.

Kwa upande wake katibu wa chama wilaya ya Mvomero Sadani Kimath alikiri kupokea barua ya mwenyekiti huyo  pamoja na ujumbe huo wa simu uliotumwa kwa mwenyekiti  huyo.

Alisema hawezi kuzungumza lolote juu ya suala hilo kwa kuwa utaratibu wa chama  hoja zote zinapelekwa kujadiliwa katika vikao na kwamba kesho ndio wanakaa kikao na watatoa maamuzi juu ya taarifa hizo.


0 comments:

Post a Comment